Diamond Platnumz Ndio Mfalme Wa Streams East Na South Africa.

SIMBA 🦁 @diamondplatnumz ameendelea kuthibitisha kuwa yeye ndiye mfalme wa muziki Afrika Mashariki na Kusini baada ya kufikisha Streams zaidi ya milioni 500 Boomplay! 👑🔥

Kwa rekodi hii, Diamond anakuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki na Kusini kufikia hatua hii kubwa, akizidi kuthibitisha nguvu yake kwenye muziki wa Afrika na kimataifa.

Safari yake ya muziki imekuwa na mafanikio makubwa, na idadi hii ya streams ni ishara ya jinsi mashabiki wake wanavyounga mkono kazi zake. Kwa kila wimbo anaotoa, Diamond anaendelea Kuweka Historia Mpya Kwa Kupata Wasikilizaji Wengi Zaidi Ndani Ya Muda Mfupi.

Hivyo Huu ni uthibitisho tosha kuwa Diamond Platnumz ndiye msanii mwenye wasikilizaji wengi zaidi Kutoka Afrika Mashariki na Kusini! 🚀🎶🔥.