Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) zimekumbushwa kuwa ukombozi wa kiuchumi ni safari ndefu na ili kuifikia nchi hizo zinahitaji mtangamano wenye nguvu na usioyumbishwa katika utekelezaji wa malengo waliyojiwekea.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa wa Zimbabwe, Prof. Amon Murwira kabla ya kukabidhi uenyekiti wa Baraza la Mawaziri la SADC kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Mhe. Rasata Rafaravavitafika jijini Antananarivo Agosti 12, 2025.
Katika Kikao hicho cha Baraza la Mawaziri, Tanzania inawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo na moja ya agenda inayojadiliwa ni maandalizi ya Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi wa SADC uliopangwa kufanyika Agosti 17, 2025.
Prof. Murwira amesema safari yoyote haikosi changamoto na kutumia jukwaa hilo kuwatahadharisha washiriki wa Mkutano huo kuwa, changamoto zisiwe sababu za kutofikiwa kwa malengo mazuri yaliyoanzisha SADC.
Alisema SADC ilianzishwa kwa lengo la mtangamano wa kikanda, nchi wanachama zinatakiwa zikumbuke hili wakati wote na kukumbuka dhamira njema ya waasisi wa Jumuiya hiyo kama vile, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Hayati Robert Mugabe na Hayati Keneth Kaunda.
Amehitimisha hotuba yake kwa kupongeza jitihada zinazochukuliwa na nchi wanachama za kuimarisha mtangamano kama vile uondoaji wa sharti la viza na usuluhishi wa mgogoro wa Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao athari zake inazikumba nchi zote za SADC.

Naye, Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Elias M. Magosi amewakumbusha washiriki wa Mkutano huo juu ya dira ya maendeleo ya Jumuiya hiyo ambayo imejikita katika maendeleo ya viwanda, kupanua mtangamano wa kikanda, biashara na masoko. Alisema lengo la mkutano huo ni kupitia utekelezaji wa dira hiyo kwa mwaka mmoja uliopita, mafanikio yaliyopatikana na kutafuta suluhu kwa pamoja katika changamoto zilizojitokeza.
Amesema mkutano huo unafanyika wakati dunia inashuhudia changamoto mbalimbali kama vile mabadiliko ya siasa za kimataifa, ongezeko la kodi katika biashara na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa misaada kutoka kwa
Leave a Reply