Man City waingia sokoni kwa hasira kusaka wachezaji

Manchester City imefikia makubaliano na klabu ya Lens kwa usajili wa beki Abdukodir Khusanov kwa ada ya pauni milioni 33.5 zaidi ya tsh. bilioni 100.

Hatua hii inaonyesha dhamira ya City kuimarisha kikosi chao katika dirisha hili la usajili.

Khusanov anayejulikana kwa uwezo wake wa kucheza nafasi mbalimbali kwenye safu ya ulinzi na anatarajiwa kuleta nguvu mpya kwenye kikosi cha Pep Guardiola. 

Usajili huu ni sehemu ya mipango kabambe ya klabu hiyo kuelekea msimu unaofuata.