Mr. Eazi Wa Nigeria Amnyooshea Mikono Diamond

Kupitia Twitter (X) Msanii Wa Nigeria @mreazi 🇳🇬 ameandika ujumbe wa kumkubali SIMBA 🦁 @diamondplatnumz na kumnyooshea mikono Star huyo kwa alichokifanya kwenye Reality Show Ya “Young Famous & African” ambayo Diamond Ametokea Kama Mhusika mkuu kwenye Show Hiyo Ya Msimu Wa Tatu (Season 3).

Kiufupi Ni Kwamba Diamond Amefanya balaa zito na kutrend kila scene, Huku wengine wakivutiwa Na Uhusika wake na jinsi anavoutawala mchezo Wa Reality Show Hiyo.

Uwezo Aliouonesha Diamond kwenye Young, Famous & African Unathibitisha kwa mara nyingine kuwa yeye ni mmoja wa wasanii wa Kiafrika wenye ushawishi mkubwa, si tu katika muziki bali pia kwenye burudani mbalimbali.