Kardinali Robert Francis Prevost kutoka Marekani amechaguliwa rasmi kuwa Kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki Duniani na atatumia jina la Papa Leo XIV.
Alizaliwa tarehe 14 Septemba 1955 jijini Chicago, Marekani, na sasa anakuwa Papa wa 267 katika historia ya Kanisa Katoliki.
Uchaguzi wake umetangazwa rasmi baada ya mchakato wa upigaji kura wa Conclave kukamilika leo. Papa Leo XIV anachukua nafasi hiyo kufuatia kifo cha Papa Francis kilichotokea mwezi Aprili
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za pongezi kwa Papa mpya kupitia ujumbe rasmi akisema:
> “Pongezi za dhati kwa Kardinali Robert Francis Prevost, Papa Leo XIV kwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani. Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninakutakia kila la kheri katika utumishi wako kwa Kanisa na Dunia kwa ujumla. Mwenyezi Mungu akusimamie na kukuongoza.”
Robert Prevost achaguliwa kuwa Papa Mpya, ataitwa Papa Leo XIV | Rais Dkt. Samia ampongeza

Leave a Reply